Pages

Powered by Blogger.

Friday, April 17, 2020

Mbinu ya majazi | Chozi la Heri


Majina mengi ya wahusika yamejengwa kimajazi ambapo majina hayo yamebeba tabia za mhusika mwenyewe.

Ridhaa; jina hili linabeba maana ya hali ya kukubali au kutosheka na jambo Fulani. Mhusika Ridhaa anakubaliana na hali ya upweke uliomkuta baada ya kufiwa mkewe Terry,mwanawe Tila,mkaza mwana wake Lily na mjukuu wake Beky. Katika kukubaliana na hali hiyo,Ridhaa anaacha kundoa majivu ya miili hiyo iliyotekea kwa moto ili kukubaliana na hali hiyo


Tenge; jina hili linarejelea kwenda kombo. Kitendo cha Bwana huyu hususan kitendo kitendo cha kuigiza wanawake ndani na kushiriki nao ufuska wakati mkewe ameenda kazini kinasawiri kabisa jina lake.

Wahafidhina; hili nalo ni jina la kimajazi likiirejelea jamii isiyotaka kubadili mtazamo wa mambo .Mwandishi ametumia jinahilo kwa kuwakatika jamii bado kuna watu wameshikilia msimamo kwamba mwanamke hawezi kupewa madaraka ya juu ya kiuongozi.

Msitu wa Heri;  hii ni ardhi iliyokuwans rutuba.Bwana Lunga-Kiriri Kangata aliweka makazi yake hapa akajikuta heri imemwangujia kutokana na kufaidi mazo ya kilimo. Hata hivyo,kitumbua kiliingia mchanga walipofurushwa na dola kwamba wanaishi hapo kiharamu.

Mwekevu Tendakazi; jina Mwekevu limetokana na nenola Kiswahili “wekeza” lenye maana ya kufanya jambo Fulani kwa lengo la kuzalisha Zaidi baadaye.Jina Tendakazi ni mwambatano wa manen “tenda” na “kazi” kwa maana ya kufanya shughuli. Mwekevu Tendakazi aliweka juhudi nyingi katika kuwainua raia alipokuwa mkurugenzi wa Shirika la Chemchemi ambazobaadaye zlizaa matunda kwa wnanchi kumwamini na kumchagua

Majina mengine ya kimajazi ni kama vile Dhahabu,Mwenge,Chandachema,Hazina,Waridi,Subira,Neema,Nyangumi,Kipanga,Tindi.

1 comments: